Enock Maregesi's Blog: Kolonia Santita (Laana Ya Panthera Tigrisi), page 6

December 3, 2017

CS-Miami






CS-Miami ni tawi la Kolonia Santita nchini Marekani. Lina watu katika miji mikubwa 78 ya Marekani, kuanzia Miami mpaka New York – mpaka Los Angeles, California. Linaongozwa na Moreno Morales, ‘El Chupacabra’, au ‘Zimwi’, mkimbizi kutoka Meksiko anayeishi Miami kinyume cha sheria toka mwaka 1988.


 


Pichani ni jiji la Miami, Florida; na jumba la Morales lililotaifishwa na Tume ya Dunia mwaka 1993, baada ya Operation DC kukamilika rasmi jijini Oslo.


 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on December 03, 2017 05:12

November 26, 2017

AKILI INAYOMTEGEMEA MUNGU INA NGUVU KUBWA KULIKO ULIMWENGU WOTE

[image error]



253. Tunapofunga na kumwomba Mungu hakuna malaika, mwema au mbaya, mwenye nguvu kuliko akili ya mwanadamu. Kwani kama uweza ni kitu cha thamani zaidi katika ulimwengu huu; hivyo, akili inayomtegemea Mungu ina nguvu kubwa kuliko ulimwengu wote. Kwa hiyo akili ya namna hiyo inaweza kutengua uchawi, inaweza kutengua kazi zote za kishetani.


Hakuna dawa ya uchawi hapa duniani. Kuna dawa ya madhara yanayosababishwa na uchawi. Kwa hiyo dawa halisi ya uchawi si kwenda kwa mganga wa kienyeji, au mchawi mwingine kutafuta tiba, au kwenda kanisani au msikitini kufanyiwa maombi, ni kuwa karibu na Mungu akilini mwako. Akili, iliyo karibu na Mungu, ina nguvu kubwa kuliko vyote ulimwenguni.




 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on November 26, 2017 15:00

November 25, 2017

Heri ya Siku ya Kuzaliwa

[image error]


Siku ya kuzaliwa ni siku ya kwanza ya safari nyingine ya siku 365, saa 5, dakika 48, sekunde 46 na maili milioni 600 kulizunguka jua. Safiri salama.


 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on November 25, 2017 05:20

November 19, 2017

Duniani Wawili Wawili

[image error]


252. Duniani wawili wawili. Umewahi kujiuliza kwa nini? Kwa nini mtu afanane sana na mtu mwingine ambaye hata si ndugu yake na labda mmoja anakaa Kagera na mwingine Tanga? Au mmoja anakaa Rwanda na mwingine Tanzania?


Nguvu za Shetani zimejificha katika sehemu za siri za mwanadamu. Kujamiiana (tendo batili la ndoa) kunautia najisi mwili wako na roho yako pia, hasa wakati wa kumwaga manii; kwa sababu dhambi zote anazofanya mwanadamu ziko nje ya mwili wake isipokuwa dhambi ya uzinzi, ambaye mungu wake anaitwa Asmodeus. Asmodeus maana yake ni Kiumbe cha Hukumu. Kutokana na dhambi ya uzinzi ndiyo maana Mungu akauhukumu kwa moto mji wa Sodoma, na miji mingine minne ya kipindi hicho.


Tunapokuwa tumelala mara nyingi tunaota ndoto tukifanya mapenzi, na watu tunaowajua au tusiowajua, hadi kileleni. Ndoto hizo ni za kishetani. Shetani hujigeuza na kuwa jini jike (Succubus) ambalo hufanya mapenzi na mwanamume kisha mwanamume kummwagia manii Succubus. Halafu Succubus huyohuyo hujigeuza na kuwa jini dume (Incubus) na kufanya mapenzi na mwanamke popote pale duniani, kwa lengo la kumwaga zile shahawa katika uchi wa mwanamke, hivyo kutia najisi mwili na roho ya mwanamke na mwanamume walioingiliwa na Incubus na Succubus kwa mpangilio huo.


Iwapo uliwahi kuota unafanya mapenzi na mwanamume, kuna uwezekano mkubwa ulifanya mapenzi na jini mahaba aitwaye Incubus; na iwapo uliwahi kuota unafanya mapenzi na mwanamke, kuna uwezekano mkubwa ulifanya mapenzi na jini mahaba aitwaye Succubus.


Succubus anapochukua shahawa za mwanamume na kujigeuza kuwa Incubus, huangalia ni mwanamke gani popote pale duniani yuko tayari kunasa mimba na bado hajafanya tendo la ndoa na mume au mpenzi wake. Kwa ruhusa ya Mwenyezi Mungu Incubus atasafiri kwa mwendo wa mwanga hadi kwa mwanamke huyo na kufanya naye mapenzi kwa njia ya ndoto, lakini lengo likiwa ni kummwagia zile shahawa alizozitoa kwa mwanamume, ili mwanamke anase mimba.


Miezi tisa baadaye, mtoto atakapozaliwa, baba halisi wa mtoto atakuwa si mume au mpenzi wa mama wa mtoto; na atafanana kivinasaba na watoto wa baba asiyejulikana, bila baba huyo au mtu mwingine yeyote yule kujua.


Lengo hasa la mpango huo ni Succubus na Incubus kunyonya nguvu za mwanamume na mwanamke (Succubus na Incubus hawanyonyi damu) hadi nguvu ziwaishe kabisa na wafariki dunia. Mtoto atakayezaliwa atakuwa na roho ya jini, atajulikana kama “cambion child”.


Kuna njia sita za kuondoa mapepo katika mwili wa mwanadamu: kwanza, kwa kukiri kwa Sakramenti; pili, kwa ishara takatifu ya msalaba au kwa kutamka Salamu ya Malaika kwa Mariamu mama yake Yesu na kwa Elizabeti mama yake Yohana Mbatizaji; tatu, kwa matumizi sahihi ya kupunga mapepo kama wafanyavyo wachungaji wengi; nne, kwa kuhamia mahali pengine tofauti kabisa na unapoishi; tano, kwa kutumia waganga wa kienyeji; na sita, kwa pepo kutengwa na mtu lakini kwa uangalifu wa watu watakatifu.


Kukiri kwa Sakramenti kunapatikana katika kitabu cha Yohana 20:21-23, katika Biblia, wakati Salamu ya Malaika Gabrieli kwa Mariamu mama yake Yesu na kwa Elizabeti mama yake Yohana Mbatizaji inapatikana katika kitabu cha Luka 1:28 na Luka 1:42 kwa mfuatano huo.


Katika njia ya nne ya kuondoa mapepo katika mwili wa mwanadamu, yaani kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine kumkimbia Succubus au Incubus, kuna tatizo. Ukihamia mahali pengine tofauti na ulipokuwa ukiishi jini litabaki mahali ulipokuwa ukiishi mwanzo, lakini litawasumbua sana wale watakaokuwa wamekuhamisha. Hivyo, mtu aliyetwaliwa na Succubus au Incubus anatakiwa kuhamishwa na wachungaji wenye uwezo wa kukemea mapepo.


Katika njia ya tano, pepo likisikia unataka kwenda kwa mchungaji ili liachane na wewe litajenga uadui na wewe. Litajenga uadui mkubwa! Ukienda lazima wachungaji wafanye maombi makali kuweza kulitenganisha na wewe, na kuhakikisha halitarudi tena kwako kwa namna yoyote ile.


Incubus wanapenda nywele! Wanasemekana kuwanyemelea sana wanawake wenye nywele za rangi ya shaba au rangi ya kimanjano! Inasemekana hutumia muda mwingi kushangaa nywele kuliko kufanya mapenzi na mwanamke. Kwa hiyo nywele nzuri, hasa za shaba au kimanjano, ni faida kwa mwanamke; lakini wale waliotwaliwa na Incubus wanatakiwa maombi.


Mtu kufanana na mtu mwingine inaweza kuwa ni kwa sababu ya muingiliano wa vinasaba vya mababu zetu (‘ancestral DNA’) lakini Succubus na Incubus ni namna nyingine ambapo mtu anaweza kufanana sana na mtu mwingine. Aidha, inawezekana kabisa kwamba kila mtu ana pacha wake sehemu fulani duniani (kutokana na mapenzi ya Mungu).


 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on November 19, 2017 15:00

November 14, 2017

Mwanasesere wa Nyoka wa Lisa Graciano

[image error]




Mwanasesere wa nyoka wa Lisa Graciano, rafiki kipenzi wa Debbie, aliyeokoa maisha ya John Murphy huko Xochimilco (‘Sochimiliko’) – Mexico City.


 


Debbie na Lisa walitoa mchango mkubwa katika vita ya Tume ya Dunia na Kolonia Santita huko Meksiko; lakini bila Mwanasesere wa Nyoka John Murphy angeuwawa, na Kolonia Santita wangeishinda Tume ya Dunia.


 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on November 14, 2017 09:24

November 12, 2017

Huwezi Kumlazimisha Mungu Afanye Kitu Unachotaka Afanye

[image error]


251. Huwezi kumlazimisha Mungu afanye kitu unachotaka afanye. Mathalani, unaweza kumpeleka mgonjwa kwa mchungaji akaombewe. Mgonjwa atapona Mungu atakapoamua apone.


Shetani ukimwomba kitu, kama umesaini naye mkataba, anakupa hapohapo. Mungu ukimwomba kitu anaweza asikupe, kwani akikupa utakuwa muujiza ambao Mungu anaufanya kwa muda anaotaka yeye, na si muda anaotaka mwanadamu. Kwa hiyo huwezi kusema kwamba Mungu anaondoa uchawi wakati hujui kama ataondoa au hataondoa.


Maria Magdalena alipomwomba Yesu afanye muujiza wa divai katika harusi huko Kana, Galilaya, Yesu alimshangaa na akasema saa yake ya kufanya muujiza ilikuwa bado haijawadia (Yohana 2:4). Mama na Mwana walikuwa na ushirika gani kati yao katika kutenda muujiza wa divai? Mama alitaka muujiza ufanyike hapohapo, lakini Mwana alikuwa na muda wake wa kuufanya muujiza huo.


Aidha, inaonekana kwamba ni mara chache sana kwamba wanaume hutolewa mapepo kwa kuomba msaada wa Mungu au sala za Watakatifu. Kwa hiyo inaonekana kwamba wanaweza tu kutolewa mapepo kwa msaada wa mapepo mengine, na ni kinyume cha sheria kutafuta msaada huo.


Mungu hakupi unachotaka. Anakupa unachostahili kupata. Wachungaji wangekuwa na uwezo wa kuondoa mapepo hapohapo, kila mgonjwa angekuwa anapona hapohapo.


Tatizo, hata hivyo, ni kwamba watu wengi hawajui kuomba! Ukiomba kitu ukapata kama ulivyoomba, kwa muda uliotaka, umepata kitu ambacho Roho wa Mungu alikuongoza kuomba. Kwa hiyo, usiache kumwambia Mungu akufundishe kuomba.


Wachungaji wanapaswa kuondoa mapepo kwa kidole cha Mungu na si kwa Beelzebuli, mkuu wa pepo.


 


 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on November 12, 2017 15:00

November 7, 2017

Sanduku la Samsonite

[image error]


Sanduku la Samsonite lililotumiwa na jambazi wa Kolonia Santita Roger Prideux, jambazi wa CS-Paris, kubebea bomu lililoisambaratisha ndege ya Shirika la Ndege la Ufaransa “Flight 279”, kama ilivyoelezewa katika kitabu cha “Kolonia Santita”.


 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on November 07, 2017 12:36

November 5, 2017

Chuki ya Mwanamke

[image error]




250. Kuna vitu vitatu katika maisha ambavyo havina kiasi katika kutenda mema au mabaya: kanisa, mwanamke, na ulimi. Kanisa na ulimi vina uwezo wa kujenga, na vina uwezo wa kubomoa kulingana na jinsi vitakavyotumika. Mwanamke anapozidisha ubaya anakuwa mbaya kwelikweli, na anapozidisha wema anakuwa mwema kwelikweli. Kwa kuwa ubavu uliomuumba mwanamke umejipinda, usilazimishe kuunyoosha.


 


Mwanamke ama apende au achukie; na akipenda anapenda kwelikweli, akichukia anachukia kwelikweli. Na machozi ya mwanamke ni machozi ya kilaghai; kwani yanaweza kutokana na huzuni ya kweli, au yanaweza kutokana na huzuni ya kilaghai. Mwanamke anapopata muda wa kufikiria, aghlabu hufikiria maovu.


 


Chuki ikizidi inazaa uchawi na hakuna uchawi mbaya kama uchawi wa mwanamke. Mwanamke ni mchawi kwa sababu ana udhaifu zaidi kiimani kuliko mwanamume, na kwa sababu lengo kuu la Shetani ni kupotosha imani, kwa hiyo Shetani anaona ni vema amshambulie mwanamke ambaye ni dhaifu kuliko kumshambulia mwanamume. Mwanamke ni mwepesi zaidi kuathiriwa na nguvu za giza kuliko mwanamume, na anapozitumia nguvu hizo vibaya anakuwa mbaya kwelikweli.


 


Lakini sababu kubwa ya mwanamke kuwa na chuki ni Hawa. Hawa ndiye binadamu wa kwanza kabisa kutenda dhambi duniani, ijapokuwa dhambi yake ilifutwa kwa baraka ya Maria Magdalena mama yake na Yesu. Dhambi ya Hawa ni dhambi ya asili. Kama ilivyo wazi kutokana na machukizo mengi ya kimwili ya mwanamke, mwanamke ana tamaa zaidi za kimwili kuliko mwanamume.


 


Hapo mwanzo wakati Mungu anaumba mbingu na nchi na vyote vilivyomo, kulikuwa na “kasoro” katika uumbaji wa mwanamke wa kwanza; kwani Hawa aliumbwa kutokana na ubavu uliojipinda wa Adamu. Kupitia kasoro hiyo mwanamke ni binadamu asiyekuwa na ukamilifu, ni binadamu hodari sana wa udanganyifu. Anapolia, mwanamke huwa anatega mtego. Huwa anakuwa na njama za kumdanganya mwanamume, kama Delila alivyomdanganya Samsoni.


 


Delila alimshawishi Samsoni amwambie kitendawili alichowapa Wafilisti, na akawapa jibu. Hivyo, Delila akawa amemdanganya mumewe.


 


Na ni wazi katika kesi ya mwanamke wa kwanza kwamba, Hawa alikuwa na imani kidogo. Kwani nyoka alipouliza kwa nini hawakula matunda ya kila mti bustanini alimwamini nyoka badala ya kumwamini Mungu, aliyesema wasile baadhi ya matunda bustanini.


 


Lakini yote haya yanaonyeshwa na elimu ya asili na historia ya neno la Kilatini liitwalo “femina”. “Femina” (“female”) hutokana na neno “fe” (ambalo humaanisha “fides” au “faith” au “imani”), na neno “minus” (ambalo humaanisha “less” au “dogo zaidi”). Kwa hiyo, “mwanamke” maana yake ni “imani ndogo”. Ndiyo maana mwanamke ni dhaifu kudumu na kushika imani, na ndiyo maana Shetani anamwonea sana.


 


Hata hivyo, dunia ni mwanamke. Bila mwanamke sisi wote tusingekuwepo. Mwanamke aliumbwa kutokana na ubavu wa mwanamume, si kutokana na miguu ya mwanamume ili mwanamume amkanyage, wala si kutokana na kichwa cha mwanamume ili mwanamume awe juu yake. Aliumbwa kutokana na ubavu wa mwanamume ili awe msaidizi wa mwanamume, chini ya mkono wa mwanamume ili mwanamume amlinde, na kando ya moyo wa mwanamume ili mwanamume ampende.


 


Kuwa mkarimu kwa mwanamke, kwani aliumbwa kutokana na ubavu uliojipinda; na sehemu iliyojipinda zaidi ya ubavu huo ni ya juu, inayofanya iendelee kujipinda daima. Maana yake ni kwamba atakuwa na chuki maisha yake yote.


 


Kwa kuwa ubavu uliomuumba mwanamke umejipinda, ukilazimisha kuunyoosha utauvunja.



 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on November 05, 2017 15:00

November 3, 2017

Taabini ya Bibi Martha Maregesi: 2017

[image error]



Taabini hii ni ngumu sana kwangu kuandika pamoja na kwamba ni miaka mitatu kamili toka giza liingie. Mwaka 2014, Novemba 4, nilimpoteza bibi yangu mpendwa, Martha Maregesi, aliyefariki dunia kutokana na ukongo wa kiharusi, na tutamkumbuka daima.


Alikuwa na roho ya kipekee; na kifo chake kiliwagusa wengi, pamoja na kwamba aliishi maisha kamili, zaidi ya siku 25550, siku 5110 zaidi, ambazo ndizo tulizopangiwa na Mungu.


Mapenzi ya mtu kwa bibi yake ni mapenzi ya kipekee. Nadhani Mungu aliwapa mabibi wote uwezo maalumu wa kuwapenda wajukuu zao, na kufanya maisha yao yatimie, kuwafanya wawe binadamu wazuri na wenye maadili mema.


Alichangia pakubwa katika malezi yangu ya utotoni; na aghalabu naweza kukumbuka nikiwa naye jikoni akipika, huku mimi nikifanya kazi nyingine, lakini wakati huohuo akinifundisha mambo kadha wa kadha ya kunikomaza kimaisha. Bibi hakuwa tu bibi. Alikuwa mlezi, rafiki na mtu aliyenihamasisha sana katika maisha.


Kifo kinaleta huzuni lakini kinaleta tumaini. Naamini bibi yangu atakwenda mbinguni, kwa sababu naamini alitubu dhambi zake akisaidiwa na wachungaji. Wachungaji hao walimtembelea kila siku, nyumbani au hospitalini, akiwa kitandani kwake akiugua. Bibi yangu alitimiza wajibu wake. Alizaliwa, aliishi, na alikufa katika toba.


Siku nitakapokufa ningependa kuzikwa jirani na alipozikwa bibi yangu, ili Yesu atakaporudi tufufuke pamoja.





 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on November 03, 2017 16:00

November 2, 2017

Amri Kumi za Mungu

[image error]




Kukiuka Amri Kumi za Mungu si dhambi ni matawi ya dhambi. Dhambi ni kumkana Mungu na kumkubali Shetani.


 


Shetani na wafuasi wake wako kifungoni sasa hivi kwa sababu dhambi walizotenda hazisameheki. Dhambi ya kumkana Mungu na kumkubali Shetani haisameheki. Kwa maneno mengine, ukimuuzia Shetani roho yako, jina lako halitaandikwa katika kitabu cha uzima litaandikwa katika kitabu cha mauti. Kama itakubidi kuuza roho, usimuuzie Shetani, muuzie Yesu.


 •  0 comments  •  flag
Share on Twitter
Published on November 02, 2017 15:15

Kolonia Santita (Laana Ya Panthera Tigrisi)

Enock Maregesi
Riwaya ya Kiswahili ya kijasusi kutoka kwa Enock Maregesi.
Follow Enock Maregesi's blog with rss.